Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
RAIS  DK.Jakaya Kikwete ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kufanya tathimini upya kwa wakazi wa vijiji vitatu wanaopisha bandari ya Bagamoyo.

Dk.Kikwete ameyasema hayo leo  Bagamoyo wakati wa kuweka jiwe la msingi la uzinduzi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ,amesema kuwa wananchi wasiondoke katika maeneo yao wakiwa na manunguniko.

Amesema kuwa mradi wa ujenzi ni mkubwa hivyo wananchi wanatakiwa kupewa haki yake kutokana na eneo ikiwa pamoja na kujengewa nyumba katika kuanza upya kwa makazi ya Kidagoni.

Rais Kikwete amesema mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo umekuja wakati mwafaka kwa kuongeza fursa nyingi baada ya kukamilika kwa mradi huo na kuongeza uchumi wa nchi.

Aidha ameiagiza Mthamini wa Halmashauri  kutafutiwa sehemu nyingine kutokana na kufanya tathimini isiyoendana na malipo hali ya wakazi hao ambao wameachia eneo hilo kwa ajili ya uchumi.

“Nchi haiwezi kuwa safi kuwepo mradi mkubwa wa bandari kubwa Afrika lakini wananchi waliocha eneo hilo wakiwa wananungunika kwa kupuchwa mali zao kwa ajili ya mtu mmoja tu”amesema  Rais Jakaya. 
 Rais Dk.Jakaya Kikwete akifungua pazia kwa kuweka jiwe la msingi la uzinduzi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo leo.
 Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha na viongozi mbalimbali baada ya kuweka jiwe la msingi na ujenzi wa  bandari ya bagamoyo leo.
Baadhi ya wananchi wa Bagamoyo waliohudhuria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.
( Picha na Emmanue Massaka wa Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...