Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Nghwira (kulia), na Mgombea nafasi hiyo kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Chifu Litayosa Yemba wakijibu maswali mbalimbali katika mdahalo wa wagombea urais ulioandaliwa na Taasisi ya Twaweza Dar es Salaam leo. Hata hivyo wagembea nafasi hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.John Magufuli na Edward Lowassa kupitia Chadema hawakuweza kuhudhuria kwa sababu mbalimbali.
Waongozaji wa mdahalo huo wakiwa kazini.
Na Dotto Mwaibale.
MGOMBEA wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli pamoja na Mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), pamoja na vyama vinaunda Ukawa, Edward Lowassa leo wameshindwa kuhudhuria mdahalo maalumu wa wagombea urais ulioandaliwa na mkimkiki kutokana na sababu mbalimbali.
Mdahalo huo ulikuwa unajadili mambo mbalimbali kama vile uchumi,katiba ya uchaguzi,malengo endelevu ya umoja wa mataifa, katiba inayopendekezwa, viashiria vya uvunjifu wa amani nchini,uchumi na huduma za kijamii kwenye sekta ya afya.
Wakizungumza kwenye mdaharo huo Dar es Salaam wagombea nafasi za urais kupitia vyama vya ACT-wazalendo, ADC na TLP walikuwa na mengi ya kuelezea kuhusu mstakari wa taifa la Tanzania.
Mgombea urais wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Chief Lutasola Yemba akijibu swali lilioulizwa kwamba wagombea hao watawezaje kuondoa rushwa kwa wanafunzi pindi wanapotafuta ajira endepo akipata ridhaa ya kuingia madarakani alisema.
SWALI
Mtawezaje kuondoa tatizo la rushwa kwa wanafunzi waliokoswa nafasi za kazi kwa maadai ya kukoswa uzoefu huku wakiombwa chochote kabla ya kupewa ajira rasmi.
Chief Yemba alisema Serikali ya ADC itahakikisha wanafunzi wanatakiwa kupata kazi punde baada ya kuhitimu masomo yao bila kusubiri kupata uzoefu huku akiwa anafanya kazi katika taaluma yake hata kama ni kwalipo kidogo na kwa baadae atakuwa na uzoefu mkubwa.
Kusoma zaidi bofya HAPA.
Kipindi hiki cha mkikiki 2015 kimejitahidi kuwezesha vyama vitoe sera zao.
ReplyDelete