Hapa ni katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambako wanawake/akina mama zaidi ya 300 wa manispaa ya Shinyanga wamekutana kujadili namna ya kupambana na ugonjwa wa Kipindupindu ambao umeukumba mkoa wa Shinyanga.Mkutano huo umeitishwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.Akina mama hao waliojitokeza kwa wingi leo jioni Oktoba 06,2015 wameweka mikakati mbalimbali ya kutokemeza ugonjwa kipindupindu ambapo Jana pekee wagonjwa 9 wamelazwa katika kambi maalum jirani na hospital ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga ambapo kati ya hao 9 wawili wamefariki dunia.


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mkutano wake na wanawake zaidi ya 300 katika manispaa ya Shinyanga uliofanyika katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine alisema wanawake ni jeshi kubwa na ni walimu wakubwa katika familia hivyo wana nafasi kubwa ya kupambana na kipindu pindu kwa kuimarisha na kuhamasisha usafi kwa akina baba,watoto na hata wanawake wenzao.
"Kipindu pindu ni hatari sana...kinaua lazima tupambane nao kwa nguvu zote..nimewaita ili kila mmoja ajue Shinyanga tuna janga..sasa kila mtu achukue hatua,ugonjwa huu unatokana na uchafu..akina mama mna nafasi kubwa sana katika hili...."alisema Matiro.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...