Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Habari katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa Jijini Mwanza katika Semina ya siku tatu iliyoanza jana Octoba 19 na inatarajia kufika tamati kesho octoba 22 ikiangazia juu ya VYOMBO VYA HABARI NA UCHAGUZI iliyoandaliwa na Chama cha cha Wanahabari Wanawake nchini Tanzania (TAMWA-Tanzania Media Women Association).

Katika Semina hiyo, imebainika kuwa katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu, Vyombo vya Habari na Waandishi wa Habari hawajaweka kipaumbele katika kuandika na kuripoti habari za Wagombea Wanawake katika nyadhfa mbalimbali nchini huku pia idadi ya Wanawake waliojitokeza kugombea katika uchaguzi huo ikionekana kuwa finyu ikilinganishwa na idadi ya Waume.

Ni kutokana na hali hiyo, Wanahabari wamehimizwa kuandika na kuripoti habari/ Matukio ya Uchaguzi mkuu kiundani zaidi kwa kuzingatia usawa kwa wagombea wote bila kujali jinsi zao hususani kuwaweka kando Wanawake huku wanawake wenyewe wakihimizwa kuwa mstari wa mbele zaidi katika kushiriki masuala mbalimbali ikiwemo ya kiuongozi katika jamii.
Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Habari katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa Jijini Mwanza katika Semina ya siku tatu iliyoanza jana Octoba 19 na inatarajia kufika tamati kesho octoba 22 ikiangazia juu ya VYOMBO VYA HABARI NA UCHAGUZI iliyoandaliwa na Chama cha cha Wanahabari Wanawake nchini Tanzania (TAMWA-Tanzania Media Women Association).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...