Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imepokea taarifa za kuwepo Mahujaji wawili kutoka Tanzania ambao wamelazwa katika mojawapo ya hospitali nchini Saudi Arabia baada ya kujeruhiwa kutokana na tukio la mkanyagano wa Mahujaji lililotokea eneo la Mina, Makkah, tarehe 24 Septemba, 2015.

Mahujaji hao ambao wanaendelea kupata matibabu na hali zao zikiendelea vizuri ni Bi. Hidaya Mchomvu na Bi. Mahjabin Taslim Khan. 
Pia kwa mujibu wa taarifa za Ubalozi Hujaji mwingine anayejulikana kwa jina la Mustafa Ali Mchira amelazwa katika Hospitali ya Ansari Madina katika chumba cha wagonjwa mahututi. Taarifa zinaeleza kuwa Bw. Mchira alipata ugonjwa tangu alipowasili Saudi Arabia na hivyo ugonjwa wake hauhusiani na ajali iliyotokea tarehe 24 Septemba, 2015. 
Vilevile, Serikali ya Saudi Arabia imeanza kutoa taarifa za alama za vidole za Mahujaji waliopata ajali. Hivyo, Ubalozi unazipitia na kuzihakiki taarifa hizo ambazo zitasaidia kuwabaini Mahujaji wetu waliokufa katika ajali hiyo. 
Kutambulika kwa Mahujaji hao waliolazwa, kunatokana na jitihada zilizofanywa na Ubalozi kwa kushirikiana na Tanzania Hajj Mission na Vikundi vya Mahujaji za kutembelea Hospitali zote zilizopo Makkah, Mina, Arafat, Muzdalifa, Jeddah na Taif kwa ajili ya kuwatafuta Mahujaji wa Tanzania waliofariki dunia au kulazwa katika hospitali hizo. 
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam

01 Oktoba, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...