Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Profesa Jumanne Maghembe akizungumza wakati wa kuzindua Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Saalam(Dawasa)jijini Arusha,katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Majisafi na Usafi wa Mazingirajiji la Arusha(Auwsa)Felix Mrema na Katibu Mkuu wizara ya Maji,Mhandisi Mbogo Mfutakamba.
Katibu Mkuu wizara ya Maji,Mhandisi Mbogo Mfutakamba akizungumza wakati wa kuzindua Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Saalam(Dawasa) jijini Arusha.

WAZIRI wa Maji,Profesa Jumanne Maghembe  amezindua Bodi  mpya ya

 Wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam(Dawasa) na kuitaka kuhakikisha wanafanyakazi kwa bidii katika mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa ili kuondoa kero ya maji kwa wananchi.


Maghembe alitoa kauli hiyo  jijini Arusha na kusema kuwa serikali imepata kiasi cha dola za Marekani 409 kutoka Benki ya Dunia,Korea Kusini na wadau wengine kuweka miundombinu ya majitaka itakayosaidia kupunguza uchafuzi wa mazingira kwenye bahari ya Hindi.


Alisema idadi ya watu katika jiji la Dar es Salaam inaongezeka kila mara hiyo serikali imejipanga kuhakikisha inatengeneza miundombinu itakayowezesha upatikanaji wa maji safi na maji taka unaondana na hadhi ya jiji.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...