Meneja uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (katikati) akiongea na mshindi aliyepatikana wakati wa kuchezesha droo kubwa na ya mwisho ya promosheni ya "Jiongeze na Mshiko" ambapo  bw.   Sylvester Lucas Boyo, mwanafunzi na  mkazi wa Shinyanga alijishindia shilingi milioni 50 na    Juma Sekele Maruka, Mwalimu mkazi wa Nyakato Mwanza    wateja wawili wa Airtel waliibuka washindi. (kushoto) ni mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha bwana Humudi Abdul Hussein  na Afisa huduma za ziada Airtel bwana Fabian Felician.(kulia) droo hii imechezwa jana katika makao makuu ya Airtel Moroco jijini Dar es saalam. 

 Afisa huduma za ziada Airtel bwana Fabian Felician akichezesha droo kubwa na ya mwisho ya promosheni ya "Jiongeze na Mshiko" ambapo  bw.   Sylvester Lucas Boyo, mwanafunzi na  mkazi wa Shinyanga alijishindia shilingi milioni 50 na    Juma Sekele Maruka, Mwalimu mkazi wa Nyakato Mwanza    wateja wawili wa Airtel waliibuka washindi. Wakishuhudia ni Meneja uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kulia) na mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha bwana Humudi Abdul Hussein (kushoto).


• Zaidi ya milioni 100 zatolewa ndani ya siku 120

Dar es Salaam, Jumanne Novemba 10, 2015, Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imewatangaza washindi wa droo kubwa na ya  mwisho ya promosheni ya “Jiongeze na Mshiko”

Airtel imekuwa ikiendesha promosheni ya “Jiongeze na Mshiko” kwa muda wa siku  120 zilizopita na kuwazawadia wateja wake wa kila wiki wa milioni 1 kwa ngazi ya Free/BURE na shilingi milioni 3 kwa wateja wa ngazi ya premium kwa gharama ushiriki wa Tshs300 tu kwa siku.


Leo “Jiongeze na Mshiko” imemzawadia Sylvester Lucas Boyo, mwanafunzi na  mkazi wa Shinyanga , shilling milioni 50 baada ya kuibuka mshindi wa droo kubwa ya mwisho wa promosheni hii.


Akizungumza wakati wa droo hiyo ya mwisho, Meneja wa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema, "leo tumefikia tamatati ya promosheni yetu ya “Jiongeze na Mshiko” ambapo mpaka sasa imezawadia wateja wetu zaidi ya shilingi milioni mia moja nchi nzima. Promosheni hii imeweza kubadilisha maisha ya wateja wetu kwa kuwazawadia pesa taslim kila wiki.

"Napenda kuwashukuru sana wateja wetu wote walioweza kushiriki katika promosheni hii ya “Jiongeze na Mshiko” tangu ilipozinduliwa mwezi Julai mwaka huu. Tunaahidi kwamba Airtel itaendelea kuwajali, kuwawezesha na kuwazawadia wateja wetu kila siku. Tutaendelea kuhakikisha tunafungua milango zaidi ya bahati kwa wateja wapya na waliokuwepo, "alisema Mmbando

Promosheni ya Jiongeze na Mshiko inaonyesha dhamira ya Airtel katika kujali wateja wake na kuwawezesha watanzania kutimiza ndoto zao, aliongeza Mmbando.

Airtel pia imemzawadia Juma Sekele Maruka, Mwalimu mkazi wa Nyakato Mwanza shilingi milioni mbili ambaye aliibuka mshindi wa mwisho wa ngazi ya Free wa promosheni hii. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...