
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini DSM,
mwenyekiti wa muda wa umoja huo PHILIP MBONDE amesema umoja huo utaweza
kuwaunganisha wapishi wa keki na wanaojishughulisha na biashara ya cake nchini
na kuweza kujumuika pamoja katika majukumu mbali mbali.
“ Hili ni jambo jipya hapa nchini, wapo
wajasiriamali wengi katika sekta hii ya keki lakini imekuwa haipewi umuhimu
sana ijapokuwa watu wengi wamekuwa wakitumia keki katika shughuli zao mbali
mbali,sasa tumeona tuanzishe umoja huu tunajua utaleta tija” alisema Mbonde.
Pia mbali na mkuu w awilaya huyo MAKONDA,
mfanyabiashara maarufu wa mau na upambaji nchini CYTHIA HENJEWELE naye
atajumuika na wapishi hao ambao wanatarajhia nae aweze kutoa elimu ya
ujasiriamali itakayowasaidia wanachama hao.
Mbonde amesema kwamba katika uzinduzi huo
wanategemea mkuu wa wilaya MAKONDA kuweza kutoa changamoto kwa wananchama wa
umoja huo kutokana na yeye kuwa kijana mwenye
kuthamini sana kazi za wajasiria mali na kujitolea katika kuhakikisha
watu wanaweza kufanikisha ndoto zao katika maisha yao ya kila siku.
Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo,amesema umoja huo
unatarajiwa kusajili ili kuwezesha
wapishi wote wa keki kuweza kupata fursa za kupata mikopo kutoka katika taasisi
za benki ili kuweza kuendeleza biashara zao na kuchangia pato la taifa kwa
kulipa kodi na kutoa ajira kwa vijana wa kitanzania ambao hawana ajira.
Mbonde amesema mpaka sasa umoja huo unawanchama hai
jumla ya hamisini ambao wanatarajiwa kushiriki katika uzinduzi huo
utakaofanyika DSM ambaoi utajumuisha wanachama kutoka mikoa mbali mbali ya
TANZANIA.
Amewaomba wadhamini mbali mbali kujitokeza kudhamini
uzinduzi huo wa chama chao kipya ambacho wanaimani kitaweza kusaidia wapishi wa
keki kuleta tija katika kazi zao.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...