Ofisa Mtendaji wa Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (Dawasco), Mhandisi Cyprian Luhemeja, akizungumza katika mkutano na wafanyakazi uliofanyika hivi karibuni Makao Makuu ya Dawasco jijini Dar es Salaam kuhusu utendaji kazi wa kazi.
 Wafanyakazi wa Dawasco wakimsikiliza Ofisa Mtendaji 
Mkuu wao.

Na Dotto Mwaibale
Ule usemi maaarufu wa "Hapa kazi tu"unaendelea kuimbwa na kufanyiwa kazi na Watanzazia wengi hususani watumishi wa Umma na serikali ili kuendana na kasi ya awamu ya Tano ya Raisi Magufuli. Kauli mbiu hiyo imekumbushwa tena na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Mhandisi Cyprian Luhemeja wakati wa kikao cha pamoja na  wafanyakazi wa shirika hilo mapema wiki hii.
“Lazima tuendane na kasi na speed ya Mheshimiwa Rais, tabia ya kufanya kazi kwa mazoea, kutojali malalamiko ya Wateja sasa ni mwisho” alisisitiza Mhandisi Luhemeja.
Aliwataka wafanyakazi kujali muda wao wa Kazi kwa kutenda yale ambayo yataondoa kero ya Maji kwa Wateja hususani kuziba mivujo ya Maji katika maeneo mengi ya Jiji pamoja na kupambana na wizi wa Maji ili kila mwananchi apate huduma ya Maji kihalali.
Alimalizia kwa kuwataka wafanyakazi wa DAWASCO kutekeleza kauli ya Rais aliyoitoa mapema wakati akifungua Bunge katika sekta ya Maji pale aliposema “LAZIMA TUWATUE KINA MAMA NDOO KICHWANI” kwa kuhakikisha huduma ya Maji inamfikia mwananchi na kuondokana na malalamiko ya upatikanaji huduma hiyo kwa maeneo stahili.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wakuu wa Dawasco, nawapongeza kwa kugundua kuwa munapaswa kwenda na kasi iliyoko sasa. Katika kuangalia hilo, naomba muangalie uwezekano wa kusambaza maji eneo la Salasala kwa Abarikiwe. Haituingii akilini sisi wakazi wa huko kukosa maji, ilihali wakazi wa salasala ya mbuyuni wao wanapata majim 24hrs. Tatizo ni nini mpaka kukosekane huduma ya maji kwa eneo hilo. Tunashawishika kuamini kuwa hayo magari yanayouza maji ni ya kwenu au mna share huko.
    Tunaomba mtusaidie tupate hiyo huduma ya maji. Mimi mkaazi wa Salasala - Abarikiwe

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...