SALAMU ZA PONGEZI

Rais wa Ireland, Mheshimiwa Michael D. Higgins amemtumia Salamu za Pongezi  Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
Katika Salamu zake hizo, Rais Higgins amesema Ireland na Tanzania zimekuwa na uhusiano mzuri na wa kirafiki kwa miaka mingi, hivyo ana matarajio kwamba katika kipindi cha uongozi wa Rais Magufuli, uhusiano huo utaimarishwa zaidi.

“Ireland na Tanzania zimekuwa na mipango ya maendeleo na ushirikiano kwa miaka mingi katika nyanja za kilimo na lishe, uimarishaji wa huduma za afya na uendelezaji wa utawala bora na uwajibikaji”, amesema Rais Higgins katika Salamu zake. 
Aidha, amesema Ireland inavutiwa na maendeleo ya kiuchumi na kijamii yaliyokwisha kufanywa na Tanzania katika miaka ya karibuni, hivyo nchi hiyo itaendeleza ushirikiano wake na Mheshimiwa Magufuli na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.   

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

20 Novemba, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...