Image result for KOSA  La  jinai

Na Bashir Yakub
Makosa  ya  jinai  ni  makosa  yote  yaliyoorodheshwa  katika  sura  ya  16  ya  kanuni  za  adhabu  pamoja  na  yale  yaliyo  katika  sheria  nyingine  kama  ile  ya  uhujumu  uchumi.  Pamoja  na  kuwapo  sheria nyingine  ambazo huorodhesha  makosa  ya  jinai   bado  Kanuni  za  adhabu  inabaki  kuwa  sheria  kuu  inayoorodhesha  makosa  ya  jinai.  Kwa  ujumla  katika  sheria tunayo makosa  makuu  ya  aina mbili. 
Kwanza  ni  hayo  ya  jinai  na  pili  ni  ya  madai.  Kwa  kusema  makosa  ya  jinai  na  madai  unajikuta  umeongelea  karibia  makosa  yote unayoyajua  na  usiyoyajua.  Kila  kosa  unalolijua  kichwani  mwako  lipo  katika   moja  ya makundi  haya.
Kwa  mifano  tu  makosa  ya  jinai  ni  kama  kupiga,  kutukana, kuendesha  kwa  uzembe( ulevi, kuongea  na simu, mwendo  kasi,kuzidisha  abiria n.k), kudhalilisha, kuiba, kubaka, kuua, utapeli, kughushi, ufisadi, rushwa, matumizi  mabaya  ya  ofisi  ya  umma, kulawiti, kumiliki  madanguro, ukahaba, dawa  za kulevya( kutumia au kuzimiliki), kuzuia  mahakama  au  mamlaka  za  kisheria  kutekeleza  wajibu, kuharibu  mali  ya  mtu, kuvamia eneo  la  mtu  kwa  nia ovu, manyanyaso  ya  jinsia  na  mengine  mengi. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...