Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo (wa pili kulia) akitembelea baadhi ya vitalu vya uchimbaji madini ya Tanzanite katika eneo la Mirelani mkoani Manyara mara baada ya kumaliza kikao kikao chake na Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite.Kulia kwake ni Afisa Madini Mkazi katika Ofisi ya Madini Mirelani, Mhandisi Henry Mditi.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo (wa kwanza kulia) akiangalia moja ya mashine zinazotumika katika shughuli za uchimbaji madini katika eneo la Mirelani mkoani Manyara wakati alipotembelea eneo hilo mara baada ya kumaliza kikao kikao chake na Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite.
Mwenyekiti wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Amos Makalla (aliyesimama) akizungumza na wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara (hawapo pichani) ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo, wa kwanza kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Manyara, Eliakim Maswi na wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa mkoa wa Arusha, Daud Ntibenda.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Omar Chambo (wa kwanza kulia) akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara ambazo zimeamua kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi.
Weka vizuri hesabu yako hapo juu usije ukaua watu kwa presha. Ni milioni ngapi?!
ReplyDelete