Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili mkoani Singida tayari kwa maadhimisho ya Miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM yanayotarajiwa kufanyika Februari 6 mwaka huu siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Namfua mkoani humo, Kauli Mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Kufanya Kazi”
Mh Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkuu wa MKoa wa Singida Dk Parseko Kone na pichani kati ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishuhudia tukio hilo.
Rais Mstaafu,Mh Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi
Mke wa Rais Mstaaafu Mama Salma Kikwete akipokelewa na baadhi ya wafuasi wa chama cha CCM mkoani humo mapema leo jioni
Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) pamoja na Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye.shoto ni Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete
Mwenyekiti wa CCM,Rais Mstaafu Dk Jakaya Kikwete akipata utambulisho kutoka kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Singida ,Mama Mary Maziku.
Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Said Amanzi.
PICHA NA MICHUZI JR-MMG-SINGIDA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...