Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imetambulisha na kuzindua kampeni yake mpya kwa wateja kupitia huduma yake yake yakifedha kwa njia ya Mtandao ya Airtel Money Kampeni hiyo imezinduliwa katika ukumbi wa burudani/club wa Maisha basement jana usiku mbele ya waandishi wa habari na watangazaji wa vipindi vya redio toka redio mbalimbali 
Meneja wa huduma ya Airtel Money Moses Alphonce akitoa sababu za ujio wa Mr. Money kwamba amekuja na habari za unafuu urahisi na usalama unaopatikana kupitia huduma ya Airtel Money sasa ambapo huwezi kupata kwingine. 
 Akiongea wakati wa uzinduzi wa Mr Money Meneja huyo alisema "Mr. Money anasema ‘tumia Airtel Money kwa kuwa ndio nafuu na hakika kuliko mitandao yote’ 
Kutuma pesa popote nchini ni BURE na kwa uhakika Lipia BILI kama LUKU na ujipatie nyongeza za unit za umeme, hii ni kwa Airtel money TU Au lipia Ving’amuzi kwa uhakika na kwa raha bila usumbufu Pia Ongeza salio popote ulipo kwa uhakika, utapata bonasi ya muda wa maongezi BURE Ukiwa na airtel money unaweza kufanya mengi Zaidi 
 Piga *150*60# SASA ujinonee.
 Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi usiku, wakati wa hafla ya kutambulisha huduma mpya ya Mr. Money, itakayomwezesha mtumiaji wa Airtel Money kurahisisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu ya mkononi.
 Meneja wa Msoko wa Airtel Money, Moses James (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa hafla ya kutambulisha huduma mpya ya Mr. Money, itakayomwezesha mtumiaji wa Airtel Money kurahisisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu ya mkononi. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando na Meneja wa Airtel Money, Asupya Nalingigwa.
Sehemu ya wafanyakazi wa Airtel Tanzania wakifuatilia jambo, wakati wa hafla ya kutambulisha huduma mpya ya Mr. Money, itakayomwezesha mtumiaji wa Airtel Money kurahisisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu ya mkononi, iliyofanyika  jijini Dar es Salaam jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...