Mkurugenzi Mkuu wa Britam Tanzania Bw. Stephen Lokonyo (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Biashara ya Bima Britam group Bw. Steven Wandera muda mfupi baada ya mkutano na waandishi wa habari katika uzinduzi rasmi wa shughuli za kampuni hiyo ya Bima hapa nchini, uzinduzi uliofanyika juzi Hyatt Regency hotel jijini Dar es salaam.
Mgeni rasmi Jaji (mstaafu) Joseph Sinde Warioba akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Britam Group Dk. Benson Wairegi muda mfupi baada ya mheshimiwa huyo kuzindua rasmi Kampuni ya Britam Tanzania inayojishughulisha na masuala ya bima katika soko la Tanzania, uzinduzi huo ulifanyika juzi katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...