Mkufunzi Nathaniel Mjema akiwasilisha mada ya kujitathmini kwa viongozi wanaoshiriki mafunzo ya uongozi yaliyowashirikisha Makatibu wakuu na wasaidizi wao.
Waratibu wa Mafunzo hayo wakifuatilia kwa kina uwashilishwaji wa mada mbali mbali zilizowasilishwa katika mafunzo hayo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum akitoa mchango katika mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya Maendeleo endelevu yaliyowashirikisha Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Serikali ya Zanzibar.
Dkt. Jochen Lohmeier kutoka Uongozi Institute akitoa mada kuhusu kuitathmini Jamii katika mafunzo ya Makatibu wakuu na Wasaidizi wao yanayofanyika Ofisi ya CAG Maisara, Mjini Zanzibar.
Washiriki wa mafunzo hayo wakibadilishana mawazo na kujadiliana kutokana na kazi waliyopewa na wakufunzi wao.
Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...