Na Sixmund J. Begashe
Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam imezindua rasmi program ijulikanayo kama Museum Arts Explosion ili kutoa nafasi kwa wasanii wa hapa nchini kufanya kazi zao za sanaa kwenye jumba hilo la Makumbusho ya Taifa kwa malengo ya kuendeleza na kukuza Sanaa na Utamaduni nchini. 
Akipokea salamu mbali mbali za pongezi kutoka ndani na nje ya nchi baada ya onesho zuri na lililo sisimu wengi waliofika kuliona kwenye Ukumbi wa Makumbusho hiyo, Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw Achiles Bufure ameeleza kuwa, wadau wengi wamependezwa sana na maamuzi haya ya Makumbusho ya kuinua uhai wa Sanaa nchini kwa kupitia Programu hii ya sasa. 
“Hii ilikuwa ni kiu ya wasanii walio wengi hapa nchini, kiu ya kuwa na sehemu watakayo oneshea kazi zao wanazo zalisha, na si kwa wasanii tu pia kwa watazania na wageni mbali mbali kwani walikuwa wakipata shida sana kuwa na mahali maalumu pakuonea sanaa za jukwaani, lakini sasa tumesha fungua milango kwa wasanii wote hapa nchini ambao watakuwa wamejiandaa vizuri kuja kujisaliji ili kuwekwa kwenye program hii mpya” alisema Bw Bufure. 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti  Msanii wa Kimataifa Bw Isack Abeneko na Bw Aloyce Makonde wameipongeza Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni kwa kuwapa heshma ya kuizindua program hio kwa wao kufanya onesho lakwanza na lililo onesha mafanikio makubwa kwa kuudhuriwa na watu wengi, hivyo wametoa wito kwa wasanii hapa nchini kuitumia nafasi hii adhimu ili kuifikishia adhira Mafundisho, Maonyo na Burudani kama yalivyo matarajio yao. 
Mratibu wa Program hiyo Bw Edgar Chatanda ameielezea program hiyo kuwa kwa sasa itakuwa ikiandaa maonesho  kila Ijumaa ya mwisho wa Mwezi ili kutoa nafasi kwa menejimenti ya Program kujidhirisha na ubora wa onesho kabla ya kupandishwa jukwaani, pia kupata muda wa kutosha wa kufikisha taarifa ya onesho hilo kwa umma ili watanzania wapate hii haki ya kuona kazi za wasanii wa hapa nchini. 
“Program hii ni endelevu, na tutakuwa na aina mbali mbali za kazi za sanaa zitakazo oneshwa hapa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni, tulikuwa na wasanii wa Dance Garage chini ya wasanii wa kimataifa, kwa kweli walifanya vizuri sana, onesho linalofuata litakuwa tarehe 29 Julai 2016 litakalo fanywa na Mwanamuziki wa Kimataifa wa Rege pamoja na Wasanii wa ngoma za ubunifu wa MUDA AFRICA, hivyo nitoe wote kwa watanzania kujitokeza kwa wingi kwenye maonesho haya kwani onesho lililopita wageni kutoka nje na watu maarufu tu ndio walio uduria”. Alisema Bw Chatanda.
 Bw Chatanda alivishukuru vyombo vya habari vyote hususani MICHUZI BLOG kwa mchango wao katika kufikisha taarifa kwa jamii kuhusiana na program hii ya Museum Art Explosion na kuviomba vyombo vya habari vingine pamoja na wadau mbali mbali kushirikiana na Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni ili kusaidia kuwapa heshama wasanii na sanaa hapa nchini.
 Msanii wa Kimataifa Bw Aloyce Makonde a.k.a Mkulima akionesha ubunifu wake wa dance alioiita MSOMI MAKOLOLI ionesha kwenye onesho la Museum Arts Explosion, Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.
 Hapo si barabarani bali ni jukwaani, wasanii wa ngoma za ubunifu Bw Tiko Mbepo alie simama kulia na Bw Isack Abeneko alieko juu ya Pikipiki wakimaliza onesho kwa kuwaacha jukwaani baadhi ya adhira walio ichukuwa na kuiweka jukwaani kama sehemu ya onesho lililofanyika kwenye Jukwa la Maonesho la Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.
 Pichani haya si masumbwi ya kweli bali ni sehemu ya ngoma ya ubunifu iliyo itwa MACHO MATATU ikichezwa na wasanii wa ngoma za ubunifu Bw Tiko Mbepo alie kushoto na Bw Isack Abeneko kulia kweye onesho la Museum Arts Explosion kwenye Jukwa la Maonesho la Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaama.
Wasanii wa kikundi cha DDI wakiwa onesha umahiri wao kwenye ngoma ya ubinifu ijulikanayo kama Freedom (Uhuru) iliyo waliyo ionesha kwenye onesho la Museum Arts Explosion, Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...