Ndege ya uzinduzi ya Shirika la Ndege la Etihad ikipokelewa na magari ya zimamoto yaliyomwaga maji kuashiria uzinduzi rasmi wa Safari za ndege kati ya jiji la Perth Australia na Abudhabi. 

Ndege ya Shirika la Usafiri wa Anga la Etihad Boeing 787 Dreamliner imetua kwa mara ya kwanza katika Jiji la Perth nchini Australia baada ya kuzinduliwa kwa safari zake rasmi ikitokea Abu Dhabi.

Ndege ya Etihad EY486 iliondoka Abu Dhabi siku ya tarehe 02 Juni muda wa saa nne na nusu usiku na kuwasili Perth mji mkubwa uliopo magharibi mwa Australia saa saba na nusu mchana ambapo ilipokelewa rasmi kwa tamaduni za uzinduzi wa ndege mpya.

Ndege ya kurudi, EY487 iliondoka Perth saa 11 jioni na kuwasili Abu Dhabi saa sita na dakika 25 usiku wa tarehe 3 Juni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...