Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Barclays Tanzania,
Abdi Mohamed (katikati), Afisa
Usambazaji wa Barclays Africa Group Limited, Vimal Kumar (kulia) na Mkurugenzi
wa Biashara Reja reja wa benki hiyo nchini, Kumaran Pather wakikata utepe
kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi jipya la kisasa la
benki hiyo lililopo katika jengo la Alpha House kando ya Barabara ya New
Bagamoyo, jijini Dar es Salaam.
Afisa Usambazaji wa Barclays Africa
Group Limited, Vimal Kumar (katikati), akifungua pazia kuashiria uzinduzi wa
tawi hilo. Pamoja naye ni Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Benki ya Barclays Tanzania, John Beja.
Mkuu wa Mtandao wa
Matawi wa Benki ya Barclays Tanzania, John Beja (mbele), akionyesha sehemu
mbalimbali za tawi jipya la kisasa la benki hiyo lililopo katika jengo la Alpha
House, kando ya Barabara ya New Bagamoyo wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa
tawi hilo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoangalia kutoka kushoto
ni, Afisa Usambazaji wa Barclays Africa
Group Limited, Vimal Kumar, Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi
Mohamed, Meneja wa tawi hilo, Nicholaus Mukanya, Mkurugenzi wa Biashara Reja
reja wa benki hiyo nchini, Kumaran Pather na Mkuu wa kitengo cha IT, Dakshit
Pandya.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya Barclays Tanzania, Abdi Mohamed (kushoto), akizungumza na
waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa tawi jipya la kisasa la
benki hiyo lililopo katika jengo la Alpha House kando ya Barabara ya New
Bagamoyo, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto kwake ni Afisa Usambazaji wa Barclays Africa Group Limited, Vimal
Kumar na Mkurugenzi wa Biashara Reja reja wa benki hiyo nchini, Kumaran Pather.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...