Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Barclays Tanzania, Abdi Mohamed (katikati), Afisa Usambazaji wa Barclays Africa Group Limited, Vimal Kumar (kulia) na Mkurugenzi wa Biashara Reja reja wa benki hiyo nchini, Kumaran Pather wakikata utepe kuashiria  uzinduzi rasmi wa tawi jipya la kisasa la benki hiyo lililopo katika jengo la Alpha House kando ya Barabara ya New Bagamoyo, jijini Dar es Salaam.
 Afisa Usambazaji wa Barclays Africa Group Limited, Vimal Kumar (katikati), akifungua pazia kuashiria uzinduzi wa tawi hilo. Pamoja naye ni Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Benki ya Barclays Tanzania, John Beja.
 Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Benki ya Barclays Tanzania, John Beja (mbele), akionyesha sehemu mbalimbali za tawi jipya la kisasa la benki hiyo lililopo katika jengo la Alpha House, kando ya Barabara ya New Bagamoyo wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa tawi hilo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoangalia kutoka kushoto ni, Afisa Usambazaji wa Barclays Africa Group Limited, Vimal Kumar, Mkurugenzi Mtendaji wa Barclays Tanzania, Abdi Mohamed, Meneja wa tawi hilo, Nicholaus Mukanya, Mkurugenzi wa Biashara Reja reja wa benki hiyo nchini, Kumaran Pather na Mkuu wa kitengo cha IT, Dakshit Pandya.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Barclays Tanzania, Abdi Mohamed (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa tawi jipya la kisasa la benki hiyo lililopo katika jengo la Alpha House kando ya Barabara ya New Bagamoyo, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto kwake ni  Afisa Usambazaji wa Barclays Africa Group Limited, Vimal Kumar na Mkurugenzi wa Biashara Reja reja wa benki hiyo nchini, Kumaran Pather.

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...