Kampuni ya Paraa Mwanga ambayo siku kadhaa zilizopita ilizindua kampeni ya Tunaangaza Afrika ambayo iliambatana na shindano ambalo litafanyika kwa miezi mitatu ambapo watu mbalimbali watakuwa wakishiriki na kushinda vitu mbalimbali ikiwepo tv, paneli ya sola, redio na king’amuzi cha Continental.

Droo ya kwanza ya kutafuta washindi imefanyika na washindi 11 kupatikana ambapo mmoja wao ameshinda tv ya nchi 24, jiko la gesi, bima ya afya ya mwaka, chaja ya simu, king’amuzi, redio na paneli ya sola na wengine wakishinda redio, flash, paneli ya sola, taa na chaja ya simu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Paraa Mwanga, Neela Krishnamurthy akimpigia simu mmoja wa washindi wa kampeni ya Tunaangaza Afrika. Kulia ni Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi.

Washindi waliopatikana katika drroo hiyo ni Lawrance Andrew, Thomas Kimanzi, Abdul Kareem, Clement Mandandi, Ramzan Niga, Issayo Matari, Majaliwa Bondala, Mohammed Issa, Juma Kitenesi na Bernard Mwalangala.

Akizungumza na MO BLOG baada ya kuwatangaza washindi wa droo ya kwanza, Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Paraa Mwanga, Mwanatumu Mohammed alisema hiyo ni sehemu ya kwanza ya kutafuta washindi wa zawadi ambazo zimeandaliwa kwa ajili ya shindano hilo na kuwataka Watanzania kushiriki kwa wingi ili waweze kushinda zawadi hizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Paraa Mwanga, Neela Krishnamurthy akizungumza na mmoja wa washindi wa kampeni ya Tunaangaza Afrika ambapo washindi 11 walipatikana katika wiki ya kwanza ya droo kufanyika. Kushoto ni Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Paraa Mwanga Mwanantumu Mohammed na kulia ni Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...