Na Mary Gwera, Mahakama ya Tanzania.
Katika muendelezo wa mafunzo ya kubadilishana uzoefu juu ya uendeshaji wa mashauri ya jinai, Majaji wanaoshiriki katika mafunzo haya wapatiwa somo juu ya Sheria ya Utakatishaji Fedha ‘Money Laundering.’
Akitoa somo hilo mapema jana, katika Ukumbi wa Hazina mjini Dodoma, Bw. Robert Kassim, ambaye ni Mwanasheria- Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu ‘Financial Intelligency Unit’ (FIU) - Wizara ya Fedha na Mipango alisema elimu juu ya Sheria hii kwa Wahe. Majaji inalenga katika kuendelea kuwajengea uelewa zaidi kutokana na kesi za aina hiyo kuletwa Mahakamani.
Mwanasheria, Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Robert Kassim akitoa somo juu ya elimu ya Utakatishaji Fedha kwa kundi la Wahe. Majaji wanaoshiriki katika mafunzo ya kuubadilishana uzoefu juu ya uendeshaji wa mashauri ya jinai yanayoendelea katika Ukumbi wa Hazina uliopo mkoani Dodoma.
“Kitengo cha Utakatishaji Fedha kinaendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wapelelezi, Waendesha Mashitaka, Mabenki na Sekta nyingine ili wote kwa pamoja tuwe na uelewa wa pamoja dhidi ya vitendo hivi haramu ambavyo huchangia katika kurudisha maendeleo ya nchi nyuma,” Alisema Bw. Kassim.
Alisisitiza kuwa suala la Utakatishaji Fedha lina madhara mengi kwa Taifa, akitaja kuwa ni pamoja na kurudisha nyuma ushindani wa kiuchumi, kushusha hadhi na utengamano wa Taasisi za kifedha na mifumo yake, pia kufifisha uwekezaji wa mitaji ya kimataifa.
Waheshimiwa Majaji wakimsikiliza mtoa mada ya Utakatishaji Fedha.
Kwa upande wake, Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Mhe. Rehema Mkuye alisema kuwa somo hilo ni muhimu sana kulielewa zaidi, akifafanua kuwa kati ya mashauri ambayo Divisheni yake itashughulika nayo ni pamoja na Mashauri ya Utakatishaji fedha na uhujumu uchumi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...