Na Evelyn Mkokoi - Bagamoyo 
SERIKALI imeiagiza Baraza la hifadhi ya Mazingira (NEMC ) na Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais kufanya tathimini ya awali ya kuangalia ni namna gani itaweza kuzuia maji ya bahari kuingia katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) na kuharibu miundombinu yake ambapo hadi sasa takribani mita 70 hadi 100 ya bahari imeisogelea taasisi hiyo. 
 Akizungumza jana wilayani Bagamoyo,Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina wakati wa ziara ya kutembelea Taasisi hiyo na kujionea ni namna gani bahari inavyosogea katika taasisi hiyo na kuanza kuathiri baadhi ya majengo. 
 Alisema kutokana na hali hiyo kuwa ya dharura ameziagiza mamlaka hizo kufanya tathimini ya awali ambapo kufikia Januari 30 mwakani watapaswa kukabidhi ripoti ya awali kwa serikali na kujua nini kifanyike katika kunusuru taasisi hiyo na kuifanya mahala pazuri pa kujifunzia masuala ya utamaduni. Mpina alisema ripoti hiyo itaweza kupelekwa serikalini ili mipango madhubuti ianze kufanyika ya kuhakikisha taasisi hiyo inakuwepo na inaendelea kutoa mafunzo yake kama kawaida bila kuathiriwa na usogelewaji wa bahari katika maeneo hayo. 
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Pamoja na ujumbe wake na Viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo wakiangalia eneo la fukwe la chuo icho ilivyoliwa na bahari ikiwa ni athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

  Eneo la Fukwe ya Bagamoyo upande wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni linavyotishiwa kuharibika vibaya kutokana na athari za mabadiliko ya Tabianchi.
 Dkt Herbert Makoye  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni ya Bagamoyo akiongea na vyombo vya habari kuhusu uhabifu wa fukwe utokanao na athari za mabadiliko ya abia nchi.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina Kiongea na Vyombo vya Habari katika fukwe ya Bagamoyo upande wa Taasisi ya Sanaa,namna ambayo majengo matatu ya chuo hicho yapo hatarini kumezwa na bahari kutokana na athari za mabadiliko a tabia nchi na kuomba msaada wa kitaalam kwa serikali hususan Ofii ya Makamu wa Rais. (Picha na Evelyn Mkokoi OMR).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...