Timu ya ya Soka ya Simba ya Jijini Dar es salaam imeendelea kujikita kileleni kwa tofauti ya alama nne baada ya Kuwabugiza Maafande wa Ruvu Shooting goli 1-0.

Mpira ulianza kwa kasi kwa upande wa Simba kutaka kupata goli la mapema lakini jitihada za mlinda mlango na mabeki ziliweza kuzaa matunda.
Mpaka kufika Dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza Simba wanaandika goli la kwanza kupitia kwa Mohamed Ibrahim baada ya kupokea pasi kutoka kwa Shiza Kichuya.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa Ruvu Shooting kutaka kusawazisha lakini safu ya ushambuliaji ilikuwa butu na haikuweza kuzaa matunda.

Kwa upande wa Simba bahati haikuwa yao baada ya kushindwa kutumia nafasi walizozipata ingawa walifanya mabadiliko.

Mpaka dakika 90 za mwamuzi Alex Mahagi zinamalizika Simba wanatoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 1-0.⁠⁠⁠⁠
Mshambuliaji wa Timu ya Simba, James Kotei akiinchambua ngome ya Timu ya Ruvu Shooting, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara duru la lala salama, uliopogwa jioni ya leo katika Uwanja wa kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda bao 1-0.
Beki wa Timu ya Simba, Abdi Banda akiwania mpira wa juu huku akimdhibiti vilivyo Mshambuliaji wa Timu ya Ruvu Shooting, Full Maganga katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara duru la lala salama, uliopogwa jioni ya leo katika Uwanja wa kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshinda bao 1-0.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...