Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati) akiweka mchanga kwenye jiwe la msingi kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mafuta na Gesi katika mji wa Kalemie. Kulia kwake ni Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia mbele) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kalemie, Kongo kwa ajili  ya kushiriki mkutano  wa kubadilishana data na uzoefu kuhusu mafuta katika Tanganyika uliofanyika hivi karibuni nchini Kongo. Nchi nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Burundi, Kongo na  Zambia. Wengine kutoka kushoto ni  Gavana wa Jimbo la  Tanganyika – Kongo, Richard Ngoy Kitangala, Waziri wa Migodi na Madini Nchini Zambia, Chris Yaluma na Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto) na Gavana wa Jimbo la  Tanganyika – Kongo, Richard Ngoy Kitangala (kulia) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Profesa Aime Ngoi-Mukena Lusa (hayupo pichani) katika mkutano huo.

 Mkurugenzi Msaidizi wa Sheria, Wizara ya Nishati na Madini, Anna Ngowi (kushoto) pamoja na wataalam wengine kutoka Tanzania wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...