KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Mwanasha Tumbo ameziagiza wilaya zote za mkoa huu kuunda majukwaa ya wanawake kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo ili yaweze kuwa chachu ya kuwakomboa kimaendeleo na kiuchumi.


Mhandisi Mwanasha ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza aliyasema hayo hivi karibuni  wakati akizindua jukwaa la wanawake mkoani Tanga ambalo litakuwa na malengo makuu ya kuwainua na kuwawezesha wanawake kiiuchumi lililofanyika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Alisema uwepo wa majukwaa hayo itasaidia kutoa fursa kwa wanawake kuweza kushiriki kikamilifu kwenye masuala mbalimbali ikiwemo kuwepo na majukumu ya kuwawezesha wanawake kuweza kujiinua kiuchumi kutokana na shughuli wanazozifanya zikiwemo za ujasiriamali.

Mmmoja wa Wajasiriamali kushoto akimuonyesha Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tangaa,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akiangalia moja kati ya bidhaa wanazozalisha wakati wa kongamano la wanawake wajasiriamali mkoani Tanga lililofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga hivi karibuni.

 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto aliyevaa hijabu ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza kulia akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...