KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Mwanasha Tumbo ameziagiza wilaya zote za mkoa huu kuunda majukwaa ya wanawake kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo ili yaweze kuwa chachu ya kuwakomboa kimaendeleo na kiuchumi.
Mhandisi Mwanasha ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza aliyasema hayo hivi karibuni wakati akizindua jukwaa la wanawake mkoani Tanga ambalo litakuwa na malengo makuu ya kuwainua na kuwawezesha wanawake kiiuchumi lililofanyika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Alisema uwepo wa majukwaa hayo itasaidia kutoa fursa kwa wanawake kuweza kushiriki kikamilifu kwenye masuala mbalimbali ikiwemo kuwepo na majukumu ya kuwawezesha wanawake kuweza kujiinua kiuchumi kutokana na shughuli wanazozifanya zikiwemo za ujasiriamali.
Mmmoja wa Wajasiriamali kushoto
akimuonyesha Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tangaa,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye
pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akiangalia moja kati ya bidhaa
wanazozalisha wakati wa kongamano la wanawake wajasiriamali mkoani Tanga
lililofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga hivi
karibuni.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa
Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto aliyevaa hijabu ambaye pia ni Mkuu
wa wilaya ya Muheza akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake
wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi
karibuni.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa
Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza
kulia akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali
wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi
karibuni.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...