Mkurugenzi wa Ajira kutoka Serikali ya Zanzibar, Bw. Amir Amir aliyeshika mike ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao cha Kamati ya kusimamia utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki akifungua kikao hicho jana kwenye ukumbi wa hoteli ya Holiday In jijini Dar Es Salaam.
Bi. Agatha Nderitu akiwasilisha matokeo ya utafiti wa namna nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zilivyotekeleza Itifaki ya Soko la Pamoja kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2014 hadi 2016. Utafiti huo ulilenga maeneo ya Soko huru la bidhaa, mitaji na uhuru wa watu kusafiri ndani ya Jumuiya. Utafiti huo ulionesha kuwa nchi za EAC zimejitahidi kutekeleza Itifaki hiyo ingawa bado kuna vikwazo na sheria zinazozuia utekelezaji wa soko hilo kikamilifu hususan kwenye vikwazo visivyo vya kibiashara.
Baadhi ya washiriki wakifuatiliwa mada kuhusu tathmini ya utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la EAC

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...