Na. Honorius Mpangala.
Ilikuwa ni katika mchezo wa ligi kuu kati ya Yanga dhidi Lipuli nilipomwona Asante kwasi akiwa amevaa 'usinga' wa nahodha. Pale pale kuna vitu vikaanza kunifikirisha nikijaribu kurejea kwenye kauli za wadau na wapenzi wa soka letu.
Kauli ambazo zinifanya akili izame huko ni katika kumbukumbu ya maneno yaliyotolewa baada ya benchi la ufundi la Simba kunadili uongozi wa wachezaji. Maneno yalikuwa dhidi ya John Rafael Bocco kupewa unahodha msaidizi nyuma ya Method Mwanjale na Mohammed Hussein. Ilikuwa katika kambi ya klabu ya Simba nchini Afrika kusini ambapo benchi la ufundi liliamua kubadili uongozi wa wachezaji.
Mabadiliko yalifanya Method Mwanjale kuwa nahodha badala ya Jonas Gerrard Mkude na kupewa wasaidizi wake .Katika orodha ya wasaidizi ilikuwa jina la John Rafael Bocco ndilo lililowafanya wapenzi na wadau walitolee hoja tofauti.
Maswali yalikuwa kwanini Bocco na sio Kazimoto au wengine waliokuwepo klabuni hapo Kwa muda mrefu. Ilichukuliwa kama ni kitu cha kushangaza sana katika tukio lile. Sababu kubwa ilikuwa kutokana na Kuvuliwa unahodha huo mchezaji mwandamizi wa klabu Jonas Gerrard Mkude.
Lakini moja ya mambo yaliyo nifurahisha ni pale Mkude alipoongea kuwa hata yeye alipopewa kuna mchezaji alivuliwa hivyo amechukulia kawaida kwake. Tukio la mabadiliko ya kiuongozi sio geni Kwa wachezaji wanaojitambua. Hapa kwetu ilionekana tofauti sana kimapokeo. Wako waliofikiria mbali zaidi na kutaka kuuaminisha umma kuwa ni maajabu ya dunia.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...