Na Karama Kenyunko, Glogu ya Jamii.


MAHAKAMA Kuu Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wazee wa baraza wa mahakama hiyo kesho wanatarajia kutoa muhtasari wa kesi ya mauaji ya bila kukusudia inayomkabili msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu anayedaiwa kumuua msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Jaji Sam Rumanyika amesema kuwa muhtasari huo utasaidia wazee wa baraza kupitia shauri hilo na kuamua kama Lulu anahatia ama la. Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa utetezi kufunga ushahidi wao kwa Stafu Sajenti, E 103  Nyagea (53) kusoma maelezo ya ushahidi ya Josephine Mushumbus ambayo aliyarekodi.

Maelezo hayo yalisomwa baada ya wakili wa utetezi, Peter Kibatala kumueleza Jaji Rumanyika kuwa wanaomba askari huyo ayasome maelezo ya Mshumbus ambaye ni shahidi wao pili kwa sababu yeye ndiye aliyemuandikia na yuko mbali hawezi kupatikana kwa urahisi. 

Akisoma maelezo hayo, amesema kuwa anamfahamu Mushumbus na ndiye aliyeandika maelezo yake ya ushahidi. Amesema kuwa katika maelezo hayo Mushumbus alijitambulisha kuwa ni Daktari, ana miaka (46) Mkazi wa Bunju National Housing na aliyaandika maelezo hayo April 23, 2012.

Akimnukuu Mushumbus, askari huyo alisoma kuwa;MShumbusi alimwambia kuwa yeye ni mmiliki ya clinic ya precious inayotoa tiba mbadala iliyopo katika jengo la Mawasiliano barabara ya Sam Nujoma.

Katika clinik yake alikuwa akitibu wateja wa aina mbali mbali akiwemo marehemu Steven Kanumba ambaye alimfahamu tangia Agosti mwaka 2011 alipofika katika clinic yake hiyo kwa Mara ya kwanza kwa ajili ya kutoa sumu mwilini, na kuanzia hapo akawa na mazoea ya kwenda hapo clinic kwa ajili ya huduma hiyo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...