Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii Dar es Salaam
Waziri wa Habari ,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe  amezindua msimu wa 16 wa Mbio za Kilimanjaro  Marathon zinazodhaminiwa na kampuni ya bia ya Kilimanjaro.

Dk Mwakyembe amesema Kilimanjaro Marathon imejizolea umaarufu mkubwa kwa kuwa maandalizi yake ni mazuri na  kuweza kuongeza idadi ya wakimbiaji mwaka hadi mwaka hali iliyofanya upatikanaji wa wakimbiaji wa timu ya taifa kuwa raisi kupitia mashindano hayo ambayo kwa sasa yanatambulika na chama cha riadha cha Dunia.

“Tunataka kuwaibua kina Felix Simbu wengine kupitia mbio kubwa kama Kilimanjaro Marathon. Nimefahamishwa kuwa Simbu pia alitokana na mbio hizi kwani aliwahi kushiriki kilometa 21 miaka ya nyuma sisi kama serikali tutafanya kila linalowezekana kuyafikia malengo haya kwa kuhakikisha kuwa mazingira yatakuwa  mazuri kwa wakimbiaji wa nadani na wa nje” amesema Mwakyembe.
Aidha Waziri Mwakyembe alitumia muda huo kuwashukuru wadhamini wengine ambao ni Tigo-21km, Grand Malt 5km na wale wa meza za maji ambao ni pamoja na First National Bank, Kilimanjaro Water, Diamond Motors Ltd, Kibo Palace, KK Security, Keys Hotel, TPC Sugar, Simba Cement na KNAUF Gypsum.
kwa upande wake Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Group, Thomas Kamphuis amesema wanajivunia kudhamini mbio za 16 za Kilimanjaro Premium Lager Marathon ambazo zinakuwa kwa kasi kubwa mwaka hadi mwaka  na hii inawapa moyo na ari ya kuendelea kuwa wadhamini wa mashindano hayo amabyo uleta mataifa zaidi ya 40 pamoja.
Amesema udhamini huu katika mbio za kilometa 42 na 5 kupitia Grand Malt, pamoja na mambo mengine unalenga kuibua vipaji zaidi katika riadha na kuwataka washiriki kujiandaa vizuri.
Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli ametoa rai kwa washiriki kuhakikisha wanajiandikisha mapema li kuepuka usumbufu dakika za mwisho na kutoa mfano wa mwaka huu ambapo namba za ushiriki zilikwisha kutokana na watu wengi zaidi kujitokeza mwishoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...