Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
WANAFUNZI 26 wamehitimu shahada ya uzamili ya Teknolojia ya habari  na Uongozi  wa katika chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Profesa Thadeo Satta amesema shahada ya uzamili  ya Teknolojia ya habari  na Uongozi inayotolewa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Avinashillingam cha nchini India.

Amesema kuwa shahada tangu imeanza kutolewa imekuwa na mwitikio kutokana na mabadiliko ya dunia ya teknolojia ya habari.

Satta amesema kuwa kuanzishwa kwa shahada hiyo nchini kwa ushirikiano chuo kikuu cha nchini  India kumewapunguzia gharama wahitaji wa shahada hiyo ambapo walitakiwa wakasome nchini India lakini wanapata kupitia Chuo cha IFM.

Aidha amesema kuwa kuwa wanashirikiana na vyuo mbalimbali katika kutoa kozi nchini kupitia chuo cha IFM.
 Makamu Mkuu wa Chuo cha Avinashillingam cha nchini India. Dk. Premavathy Vijayan akizungumza katika mahafali ya 11 ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Thadeo Satta akizungumza katika mahafali ya 11 ya shahada ya uzamili waTeknolojia ya Habari na Uongozi leo jijini Dar es Salaam.
 Wanafunzi 26 wakitunukiwa shahada ya uzamili waTeknolojia ya Habari na Uongozi katika mahafali ya 11 Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), leo jijini Dar es Salaam.
 Mhitimu wa shahada ya uzamili waTeknolojia ya Habari na Uongozi,     Edwin Owawa akitunukiwa cheti  katika mahafali ya 11 Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), leo jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mkuu wa Chuo cha Avinashillingam  cha  nchini India.Dk. Premavathy Vijayan akiwa katika picha ya pamoja ya Watendaji wa IFM na Wahitimu 26 katika mahafali ya 11 ya Chuo cha IFM leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...