MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, wametakiwa kujiunga na huduma ya akaunti ya akiba ya fahari ambayo ni jibu kwa kila mtanzania kuweka akiba na kufikia uhuru wa kibenki. 
Meneja wa benki ya CRDB Tawi la Kiteto, Lucy John akizungumzia huduma ya akaunti ya akiba ya fahari kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto alisema huduma hiyo ni muhimu kwa jamii. 
Lucy alisema pia huduma ya SIMAccount ambayo ni rafiki na nafuu kwa kila mwananchi unaweza kujiunga kwa kubonyeza *150*62#Ok! 
Alisema pia huduma za insurance zinapatikana kwenye Tawi la CRDB, bima za magari, pikipiki, nyumba za makazi, hoteli na mazao ambayo yapo kwenye maghala. 
Meneja wa Benki ya CRDB wa Mkoa wa Manyara, Ronald Paul aliwaeleza madiwani hao juu ya ukarabati wa hospitali ya wilaya ya Kiteto.
Paul alisema anatambua fika kuwa madiwani wa halmashauri hiyo ya Kiteto na watumishi wao ni wateja wazuri wa benki hiyo hivyo wataendelea kushirikiana kwa  mbalimbali katika ujenzi wa Taifa.
 Meneja wa Benki ya CRDB Mkoa wa Manyara Bw.Ronald Paul akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto.
 Meneja wa Benki ya CRBD Tawi la Kiteto Mkoani Manyara Bi. Lucy John akizungumza juu ya huduma ya akaunti ya akiba ya fahari kwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto. 

Meneja wa Benki ya CRDB Mkoa wa Manyara Bw. Ronald Paul akiendelea kueleza juu ya ukarabati wa hospitali ya wilaya ya Kiteto kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...