Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeombwa kusaidia uzalishaji wa zao la chai wilayani Lushoto mkoani Tanga ili kuchagiza shughuli za kiuchumi na kunyanyua kipato cha wakulima wadogo wadogo wilayani humo humo.

Ombi hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. January Lugangika wakati akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine alipotembelea Ofisini kwake.

Bw. Lugangika alisema kuwa Serikali imejipambanua katika kukufua viwanda hasa vyenye kusaidia wakulima wadogo wadogo kupitia ununuzi wa malighafi akilitaja zao la chai kuwa ni la kipaumbele katika kuchagiza juhudi hizo za Serikali.“Benki ya Kilimo ikisaidia kufufua viwanda vyetu vya chai itawanufaisha wakulima wetu wanaolima chai hivyo kuweza kunyanyua kipato cha wakulima wilayani kwetu,” alisema.

Aliongeza kuwa wilaya ya Lushoto imejaliwa kuwa na eneo kubwa la uzalishaji zao la chai hivyo kuongeza tija katika kuendeleza zao hilo.Akizungumza wakati wa kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine alisema TADB ipo tayari kuchagiza uzalishaji wa mazao ya kimkakati yenye masoko ya uhakika ikiwemo zao la chai na yenye kulenga kunyanyua hali za maisha ya wakulima wadogo wadogo nchini.
 Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. January Lugangika (wapili kushoto) akizungumza na ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ulipomtembelea Ofisini kwake wilayani Lushoto kuzungumzia fursa za uwekezaji katika kilimo. Wanaomsikiliza ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kushoto), wengine ni Afisa Biashara Mwandamizi wa TADB, Eunice Mbando (kulia) na Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo, Bw. Tito Kayugyuma (wapili kulia).
IMG_7031
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. January Lugangika akihimiza jambo wakati wa kikao.
IMG_7032
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine akifafanua jambo wakati akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. January Lugangika (hayupo pichani).
IMG_7033
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kulia) akiwa katika mazungumzo na Katibu Tawala wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Nicodemas Tambo (katikati). Anayesikiliza ni Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo, Bw. Tito Kayugyuma (kushoto).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...