Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MAKOSA mbalimbali ambayo yanafanywa na wanaoendesha vyombo vya moto barabarani yamesababisha Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kupata zaidi ya Sh.Bilioni 2.74.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amesema hayo leo ambapo amefafanua jeshi hilo linaendelea na operesheni ya kuwasaka madereva wa magari na watumiaji wa vyombo vya moto ambao hawazingatii sheria ya usalama barabarani.

Amefafanua katika operesheni hiyo wamefanikiwa kukamata magari madogo,maroli, pikipiki na daladala ambapo wahusika wametozwa faini ambapo zaidi ya Sh.Bilioni 2.74 zimepatikana.

Pia amesema kuwa ni vema madereva kuhakikisha wanafuata sheria za usalama barabarani huku akionya tabia ya baadhi ya madereva wanaondesha magari huku wakichati muda wote.

Amesema ni vema wakaacha tabia ya kuendelea kutumia simu kwani madhara yake ni makubwa na ni sawa na kukitafuta kifo.

Pia Kamanda Mambosasa amewawataka watu ambao wametozwa faini za barabani kulipa kwa wakati kwani kuna tabia ya kulimbikiza deni na wataendelea kuwasaka wadaiwa wote na iwapo watashindwa gari litachukuliwa na kuwekwa Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...