Mwili wa aliyekuwa Mmiliki na Mwanzilishi wa Timu ya Tukuyu Stars (Banyambala) Ramneck Patel(Kaka) aliyefariki octobar 18 nyumbani kwake alipokuwa akiendelea na matibabu baada ya kuruhusiwa kutoka katika hospital ya Kanda ya Rufaa ya Mbeya alikokuwa akipatiwa matibabu, umewasili nyumbani kwake majira ya saa 4 asubuhi kwa ajili ya taratibu za mazishi.

 Taarifa za ndugu wa marehemu kuhusu taratibu za mazishi zinasema, Mwili wa marehemu Baada ya kufanyiwa Ibada Nyumbani kwake leo Oktoba 24,2018, utapelekwa viwanja vya Sokoine -kwa wananchi ndugu jamaa na kuaga na baadaye kusindikizwa katika nyumba yake ya milele Makaburi ya sabasaba jijini Mbeya, ambapo kwa mujibu wa dhehebu la Baniani mwili huo utachomwa kama sehemu ya taratibu za mazishi. 

 Klabu hiyo ilianzishwa mwaka 1980 na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu wakati huo ikiitwa daraja la kwanza bara mwaka 1985 -86 na baada ya mwaka mmoja ikashuka daraja. 
 Mwili wa aliyekuwa Mmiliki na Mwanzilishi wa Timu ya Tukuyu Stars (Banyambala) Ramneck Patel(Kaka) ukiandaliwa mapema leo nyumbani kwake kwa ajili ya sala na baadae   kwa ajili ya taratibu za mazishi.
 Gari iliyobeba mwili wa aliyekuwa Mmiliki na Mwanzilishi wa Timu ya Tukuyu Stars (Banyambala) Ramneck Patel(Kaka) ukiwasili yumbani kwake kwa ajili ya sala na baadae   kwa taratibu za mazishi.
 Kikosi cha Timu ya Tukuyu Stars wakati huo alipokuwa akiisimamia,na yeye akiwemo pichani kulia enzi za uhai wake.
 Mwili wa aliyekuwa Mmiliki na Mwanzilishi wa Timu ya Tukuyu Stars (Banyambala) Ramneck Patel(Kaka) enzi za uhai wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...