Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza wakurugenzi kushirikiana na madiwani kuhakikisha suala la kupunguza udumavu katika mkoa wa Rukwa linakuwa ni ajenda ya kudumu katika vikao vya mabaraza ya madiwani pamoja na mikutano ya hadhara katika kuwaeleimisha wananchi juu ya athari ya udumavu.

Amesema kuwa suala la udumavu lisisahaulike pindi tunapoangalia ufaulu wa watoto wetu mashuleni, na kuwa mstari wa mbele kutoa ahadi za kuhakikisha watoto wanaongeza ufaulu huku udumavu ukiwa bado haujashughulikiwa.

“Tuone kwamba kama huna hali mbaya ya matokeo ya kielimu yanachangiwa pia na udumavu kwasababu udumavu umekuwa wa muda mrefu na kama tunaukubali upo, sasa kwanini usikubaliane pia na matokeo yanayotokea, tuweke jitihada kubwa sana kuondoa udumavu ili watoto wetu waongeze ufaulu,” Alisisitiza.

Ameongeza kuwa kama si hivyo basi itabidi takwimu udumavu ziangaliwe upya, ama kama kwenye elimu kuna kupasi sana basi kuna wizi wa mitihani ama kuna wageni wengi sana wanaotoka nje kuja kusoma Kwetu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...