MTAWALA wa Ras al Khaimah Shaikh Saud Bin Saqr Al Qasimi amemuhakikishia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kuwa serikali yake itatoa ushirikiano katika kufanikisha shughuli ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia kupitia Mkataba uliosainiwa hapo jana.
Shaikh Saud Bin Saqr Al Qasimi aliyasema hayo leo wakati alipokuwa na mazungumzo na mwenyeji wake Rais Dk. Shein katika ukumbi wa Ikulu mjini Zanzibar, ambapo katika mazungumzo hayo Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd alihudhuria pamoja na viongozi wa Ras al Khaimah na wa Zanzibar.
Katika maelezo yake, Shaikh Al Qasimi alisifu juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Kampuni ya RAK GAS ya Ras al Khaimah katika kutekeleza mipango iliyopo ya utafutaji wa nishati hiyo.
Katika mazungumzo hayo, Mtawala huyo alieleza kuvutiwa kwake na mipango inayoendelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya mafuta na gesi hasa kwa maamuzi yaliyofikiwa ya kutaka kujenga bandari maalum ya mafuta na gesi katika eneo la Mangapwani.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...