*Aagiza wakae na wakandarasi wao na kupima kama watamaliza kazi
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amekutana na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye
eneo la tenki la maji la kutolea huduma katika ujenzi wa mji wa Serikali
Mtumba badala ya ukumbi wa Hazina kama alivyokuwa amepanga awali.
Akiwa
Ihumwa, Waziri Mkuu amewaagiza Mawaziri wafike kwenye maeneo ya ujenzi
wa ofisi zao, watathmini uwezo wa wakandarasi wanaojenga majengo ya
wizara na pale watakapojiridhisha kuwa uwezo wao ni mdogo, wawabadilishe
mara moja.
Ametoa agizo hilo leo mchana (Ijumaa, Desemba 28, 2018) akiwa
kwenye kikao cha kazi (site meeting) na mawaziri 15 na manaibu mawaziri
katika eneo la Ihumwa lililoko km. 17 kutoka jijini Dodoma.“Mawaziri mliopo na makatibu wakuu wote kaeni na wakandarasi wenu hapa site ili waeleze kazi hii itakamilishwa lini. Lengo letu ni kuhakikisha kuwa kazi hii inakamilishwa kwa wakati,” amesisitiza.
Waziri
Mkuu ametumia fursa hiyo kuwapa mrejesho Mawaziri juu ya changamoto
alizokutana nazo jana alipofanya ukaguzi wa ujenzi kwa kila wizara.
“Nataka Mawaziri ambao ofisi zao zinajengwa wa watu wa Mzinga, wakae nao
na kutathmini uwezo wao na kama mtaona hawawezi, mkabidhi kwa
mkandarasi mwingine,” amesema Waziri Mkuu.
Amewataka
wakandarasi wahakikishe wanaongeza idadi ya vibarua ili kazi hiyo iweze
kwenda haraka. “Wizara iliyofanya vizuri kuliko zote ni ya Utumishi,
wao wako hatua nzuri. Kwa maana ya uchapaji kazi, eneo nililokuta lina
wafanyakazi wengi ni magereza,” amesema.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Waziri wa Elimu, Sayansi na
Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati alipowasili kwenye eneo la
Ihumwa jijini Dodoma, unapojengwa Mji wa Serikali kukutana na Mawaziri
na Makatibu Wakuu, Desemba 28, 2018. Wengine pichani kutoka kushoto ni
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -
TAMISEMI, Selemani Jafo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.
Philip Mpango na kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,
Vijana na Ajira, Anthony Mavunde. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye eneo la Ihumwa jijini Dodoma unapojengwa mji wa Serikali, Desemba 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dkt. Maulid Banyani baada ya kuzungumza na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye eneo la Ihumwa jijini Dodoma unapojengwa Mji wa Serikali, Desemba 28, 2018. Katikati ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi baada ya kuzungumza na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye eneo la Ihumwa jijini Dodoma unapojengwa mji wa serikali, Desemba 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye eneo la Ihumwa jijini Dodoma unapojengwa mji wa Serikali, Desemba 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Dkt. Maulid Banyani baada ya kuzungumza na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye eneo la Ihumwa jijini Dodoma unapojengwa Mji wa Serikali, Desemba 28, 2018. Katikati ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi baada ya kuzungumza na Mawaziri na Makatibu Wakuu kwenye eneo la Ihumwa jijini Dodoma unapojengwa mji wa serikali, Desemba 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...