Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mojawapo ya mashine iliyopo katika karakana ya wakala huo mkoa wa Njombe wakati wa ziara yake ya kukagua utendaji kazi, kushoto ni Kaimu Meneja wa Temesa Mkoa wa Njombe Mhandisi Saidi Mawazo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiichunguza mashine ya kuchongea vipuri vya mitambo mbalimbali wakati akikagua chumba cha kuhifadhia mashine hizo katika karakana ya mkoa wa Mbeya. Kulia ni Meneja wa TEMESA mkoani humo Mhandisi Sunday Kyungai.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Katavi Mhandisi Stembrige Rushatila katikati akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto eneo la karakana wanapotegemea kupaboresha ili kuongeza uzalishaji wakati wa ziara ya mtendaji mkuu kukagua miundombinu ya karakana za wakala.  
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Iringa Mhandisi Ian Makule kulia akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle mashine ya kisasa ya kutoa na kubadilishia matairi ya magari iliyopo katika karakana ya mkoa huo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TEMESA mkoa wa Iringa mara baada kuzungumza nao na kusikiliza changamoto wanazokutana nazo katika utendaji kazi. Kulia kwake ni Meneja wa TEMESA Mkoani humo Mhandisi Ian Makule.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akitoa msisitizo wakati akizungumza na wafanyakazi wa wakala huo mkoani Rukwa alipokua ziarani kukagua utendaji kazi. Pembeni yake ni Meneja wa Mkoa huo Mhandisi Fidol Tumbi.PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO - (TEMESA)

Posted: 24 Feb 2019 11:30 AM PST
  Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akionesha hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa tenki la maji ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.
 Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akionesha hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la Wizara ya Nishati linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara yakukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.
 Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akionesha hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la Wizara ya Fedha na Mipango linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara yakukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.
 Muonekano wa hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora katika mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma. 
  Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akiongea na mafundi katika jengo la Ofisi ya Makamu wa Rais linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara yakukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.


 Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akiongea na Mkandarasi na Mshitiri katika jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...