Hussein Stambuli, Morogoro

SERIKALI mkoani morogoro imewachukulia hatua baadhi ya watumishi wa sekta ya afya kwa kuwahamisha vituo baada ya kukithiri kwa malalamiko ya tuhuma za rushwa, lugha chafu na utendaji mbovu akiwemo Mganga Mkuu na Muuguzi Mkuu wa Mkoa huo.
  
 Akizungumza na waandishi wa habari,Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro  Cliford Tandari amesema uhamisho huo utahusisha Mganga mkuu wa mkoa, Muuguzi Mkuu wa mkoa, Mganga Mkuu wa meno wa Mkoa pamoja na watumishi wa idara mbalimbali zilizopo katika sekta hiyo.

"Kufuatia ziara ya Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Dk.Gwajima baada ya kufanya ukaguzi katika halmashauri zote mkoani hapa sasa imebainika kumekuwa na viashiria vya rushwa, hali mbaya ya utoaji huduma kwa wagonjwa, majibu mabovu yanayotolewa na wauguzi.

"Sisi kama Serikali tumeamua kuingia kati suala hili na kuhakikisha huduma za afya mkoani hapa zinatolewa kwa usawa, haki na uboraa,"amesema Katibu Tawala huyo.


Watumishi hao watapangiwa maeneo mengine ya kazi nchini huku Serikali ikiahidi kufuatilia mwenendo wao wa kazi mahali popote watakapokuwa kwani lengo ni kuhakikisha watumishi wa umma wanakuwa msaada mkubwa kutatua kero za wananchi.
Katibu tawala mkoa wa morogoro, Cliford Tandari akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro kuhusu watendaji wa sekta ya afya ya mkoa huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...