Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi (kulia) akizungumza naWaziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. GeorgeBoniface Simbachawene (kulia) alipomtembelea Ofisini kwake Vuga VisiwaniZanzibar kwa ajili ya kujitambulisha.





Mratibu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Khalid Bakari Hamrani(wa pili kulia) akimpa maelezo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa RaisMuungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene kuhusu ujenziunaoendelea wa jengo la Kituo cha Afya Kianga Wilaya ya Magharibi A MkoaniMjini Magharibi unaojengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) nakusimamiwa na wananchi wenyewe. Kulia ni Mkurugenzi wa Muungano Ofisi yaMakamu wa Rais Lupi Mwaikambo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. GeorgeBoniface Simbachawene akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi waKituo cha Afya cha Kianga Wilaya ya Magharibi A Mkoani Mjini Magharibiunaojengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na kusimamiwa nawananchi wenyewe.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. GeorgeBoniface Simbachawene akizungumza alipotembelea eneo la Kilimani mjiniZanzibar kwenye mradi wa miti ya mikoko kando ya Bahari ya Hindi ili kuhifadhimazingira ikiwa ni sehemu ya ziara yake. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara yaMazingira Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Farhat Ali Mbarouk.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. GeorgeBoniface Simbachawene akizungumza na watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Piliwa Rais wa Zanzibar alipotembelea Ofisi hiyo kujitambulisha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...