Naibu waziri wa Wizara ya Maji Mh Juma Aweso, akizungumza mara baada ya kutembelea Banda la Maonyesho la Baraza la Kilimo Tanzania katika viwanja vya Maonyesho ya wakulima nanenane Kanda ya Mashariki yanayofanyika Mkoani Morogoro.

Baraza la Kilimo Tanzania kuhakikisha linawasaidia wakulima ili wapate taarifa sahihi kuhusu pembejeo hasa mbegu ili waweze kuzalisha kwa tija.
Mh Aweso amesema hayo Agosti 05 mwaka huu mara baada ya kutembelea Banda la Baraza la Kilimo Tanzania katika Maonyesho ya wakulima kanda ya Mashariki yanayofanyika viwanja vya Mwl Nyerere Mkoani Morogoro.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi wa zamani Omary Mahita akifurahia jambo na washiriki wa maonyesho ya wakulima ndani ya Banda la Baraza la Kilimo Tanzania, pia alipata fursa ya kupata maelezo ya kina juu ya bidhaa ya mchele ya Rukwa Super Rice  inayozalishwa na wakulima hao bila kutumia mbolea za kisasa.
 IGP wa zamani Omary Mahita afurahishwa na juhudi za Baraza la Kilimo Tanzania katika kuwawezesha wakulima wanawake, katika picha akiagana na mkulima wa korosho kutoka Mtwara ambaye yuko ndani ya Banda la Baraza la Kilimo.
 Mratibu wa Programu ya Ubia wa KIlimo Tanzania chini ya Baraza la Kilimo Bw. Mark Magila akipata maelezo ya bidhaa zinazoonyeshwa na mshiriki wa maonyesho ya Kilimo mwaka 2019,ndani ya Banda la Baraza la Kilimo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...