Mratibu Taifa wa Programu ya Ubia wa Kilimo Tanzania chini ya Baraza la Kilimo Bw. Mark Magila akifungua Warsha ya siku moja iliyofanyika Mkoani Morogoro na kujumuisha Wadau wa Kilimo ilikujadili matokeo ya Utafiti kuhusu Mfumo wa uagizaji Mbolea kwa Pamoja. 
 Makamo Mwenyekiti wa Chama cha wasambazaji wa Pembejeo nchini TADCOS Bw. Iddi Madeni akichangia kuhusu Mfumo huo wa uagizaji wa Mbolea kwa pamoja, ambapo pamoja na masuala mengine amesema ni muhimu serikali ikawa inawashirikisha kabla ya upangaji wa bei elekezi .
 Mkulima wa Tumbaku kutoka Wilayani Chunya Mkoani Mbeya Bw. Juma Phesto akichangia mada kuhusu uagizaji wa Mbolea kwa pamoja ambapo amekiri kuwa mfumo huo umesaidia mbolea kuwafikia wakulima kwa wakati, Mkutano huo umefanyika Mkoani Morogoro.
Sehemu ya washiriki wa Warsha hiyo ya siku moja iliyoandaliwa na Baraza la Kilimo Tanzania wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa mada katika mkutano huo uliofanyika Mkoani Morogoro.
 Washiriki wa Warsha ya wadau wa Kilimo iliyofanyika Mjini Morogoro na kuratibiwa na Baraza la Kilimo Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa warsha hiyo.


SERIKALI imeelezea kuridhishwa na mfumo wa uagizaji wa Mbole kwa pamoja licha ya uwepo wa changamoto kadhaa zikiwemo za ucheleweshaji wa mbolea kuwafikia wakulima ikiwa ni pamoja na suala la bei elekezi.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa jana Mjini Morogoro na Afisa Kilimo Idara ya Mazao Kitengo cha Pembejeo kutoka Wizara ya Kilimo Bw Joseph Lyafwila wakati wa Warsha ya wadau wa Sekta ya Kilimo iliyokuwa ikiangazia matokeo ya utafiti uliofanywa kuhusu Mfumo wa uagizaji wa Mbolea kwa Pamoja ulioandaliwa na Baraza la Kilimo Tanzania.

“Kwetu kwenye Sekta ya Kilimo Mfumo huu ni mpya na tayari  tumeona mafanikio yake ndani ya kipindi cha miaka mitatu, hivi sasa Mbolea inafika nchini kwa wakati na wakulima pia inawafikia kwa wakati na kama nilivyosema ni ukweli kwamba bado kunachangamoto kadhaa,

“Tunajua pia wakulima wamekuwa wakilalamikia suala la bei na hii inatokana na ukweli kwamba kuna baadhi ya vijiji viko mbali sana na inafanya bei inapanda kidogo inagwa Serikali bado inangalia changamoto zote  zinazoendelea kujitokeza katika mfumo huu ili tuweze kuzishughulikia “ alisema Bw Joseph.

Mkurugenzi wa Sera, Mipango na Utetezi kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Bw. Timothy Mmbaga alisema kuwa waliamua kufanya utafiti huo kuhusu maendeleo ya mfumo ili kuona namna inavyoweza kuishauri Serikali namna bora zaidi ya kuendelea na mfumo huo.

“Kabla ya mfumo huu kulikuwa na changamoto nyingi sana watu walikuwa wanauziwa mbolea feki wengine walikuwa wanauziwa hadi siment, lakini Baraza la Kilimo tulipiga sana kelele na tunaishukuru Serikali ililiona hili na hatimaye kuja na mfumo huu,

“Tunajua mahitaji ya mbolea kwa sasa yanazidi kuongeka hivi sasa inakadiriwa kufikia tani laki nne ingawa kupitia mfumo huu ni tani 70,000 pekee ndio inayoagizwa ingawa tunajua kuna njia nyingine nyingi za uagizaji wa mbolea zaidi ya DAP na UREA zinazoagizwa kupitia mfumo huu” alisema Bw. Mmbaga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...