Na Luteni Selemani Semunyu CHINA.
Bondia Koplo Selemani Kidunda maarufu ‘Mtu Mbaya’ ameendeleaza ubabe baada ya kutinga hatua ya robo fainali katika Mashindano ya Dunia ya Majeshi katika Mchezo wa Ngumi nchini China
Kidunda ameingia hatua hiyo baada ya kumtwanga kwa pointi Munkhajar BatBaatar wa Mongolia na kupata alama 10 kutoka majaji wote Watano katika mpambano huo.
Bondia huyo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania alitinga hatua hiyo ya pili baada ya kwanza kumpiga kwa KO bondia Dapura Liyanage PRK kutoka Srilanka katika raundi ya pili ya mchezo.
Wakati mpinzani wake alitinga hatua hiyo baada ya kumpiga Bondia Aung ye Win kutoka Mnyamar kabla ya kukutuna na kidunda alieyemuondosha katika mashindano hayo.
Sasa Kidunda anasubiria Mpinzani atakayepambana nae mara baada ya kumalizika kwa mapambano ya leo usiku na kuamua mabondia watakaoingia katika hatua ya robo fainali ambao anaefuvu anajihakikishia medali.
Akizungumza mara baada ya Mchezo Kidunda alisema mashindano bado ni Magumu kwani kila Nchi imeajiandaa lakini dua za Watanzania zimekuwa msaada mkubwa na kuomba kuendelea kumuombea.Naye Kocha wake Hasan mzonge amesem,a amefurahishwa na hatua aliyofikia na matumaini yake atafanya vizuri katika hatua zinazofuata amabazo ni ngumu lakini ni zenye mafanikio Makubwa.
Mmoja wa Viongozi katika Msafara timu inayowakilisha Tanzania Kapteni Mohamed Kasui amesema katika mashindano makubwa kama haya kufikia hatua hiyo ni mafanikio makubwa na wanazidi kumuombea kidunda kufanya vizuri…
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...