Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

ABIRIA waliokuwa wakisafiri na basi la Majinja lenye  namba T 619 DCF wamenusurika kifo baada basi hilo kupata ajali katika eneo la Mlima Kitonga mkoani.

Ajali hiyo imetokea leo na kusababisha taharuki waliokuwa wakisiri na basi hilo ambapo hata hivyo baadhi ya abiria wamepata majeraha na hakuna aliyepoteza maisha kutokana na ajali hiyo.

Wakizungumza na Michuzi TV na  Michuzi Globu ya jamii, baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema baada ya kutokea kwa ajali hiyo walitoa msaada wa kuwatoa abiria waliokuwa ndani ya basi hilo.

Baadhi ya abiria wametolewa kupitia madirishani kutokana na kwamba basi hilo kilikuwa limepinduka kwa magurudumu kuwa juu na paa la basi kuwa chini.

Kwa mujibu wa mashuhuda hao walioamua kutoa msaada kwa abiria hao, wamesema jambo la kushukuru Mungu ni kwamba hakuna aliyepoteza maisha ila kuna baadhi ya abiria wamepata majeraha madogo.

"Kwa kweli tunashukuru hakuna aliyepoteza maisha katika ajali hii,tumefanikiwa kuwatoa wote waliokuwa ndani ya basi la Majinja.Ila kuna baadhi ua abiria wamepata majeraha. 

"Kwa sasa tunawaona wako vizuri sijui labda kama kutakuwa na abiria ambaye amepata majereha kwa ndani,"amesema mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo.
 
Hata hivyo Michuzi Globu na Michuzi TV inaendelea kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa ili kuzungumza ajali hiyo na hali za majeruhi.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...