Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amezindua mfumo wa kuratibu na kusimamizi miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye Mkoa huo kwa njia ya mtandoa kwa lengo kuongeza Chachu na kasi ya uwajibikaji kwa Viongozi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa taarifa sahihi za miradi ya maendeleo jambo litakalopunguza tatizo la miradi kusuasua.

RC Makonda amesema kwa muda mrefu baadhi ya Watendaji walikuwa wakitoa taarifa za wongo kwa viongozi kuwa mradi unaendelea vizuri na upo katika hatua nzuri lakini kiongozi anapofika kwenye eneo husika anakuta hakuna kinachoendelea lakini kupitia mfumo huo kiongozi ataona kila kitu kinachoendelea kwenye mradi kwa kutumia Computer au Simu ya mkononi.

Aidha RC Makonda amesema ndani ya mfumo huo zitapatikana taarifa zote muhimu za miradi ikiwemo Msimamizi wa Mradi, Mkandarasi, Gharama za mradi, Muda wa mradi kukamilika, fedha iliyolipwa, hatua mradi ulipofikia pamoja na Mamlaka ya serikali ya mtaa ambapo mradi husika unatekelezwa.

RC Makonda amesema faida za mfumo ni pamoja kuongeza Uwazi, uwajibikaji wenye tija.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...