Tanzania imesema itatumia kipindi chake cha uenyeketi wa nchi za Afrika,Caribbean na Pacific na Umoja wa nchi za Ulaya katika kusisitiza juu ya urejeshwaji wa rasilimali zilizoporwa katika nchi hizo nyakati za ukoloni,kuheshimu mamlaka ya nchi husika na urejeshwaji wa wahamiaji haramu kwa kuzingatia utu na haki za binadamu.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. damas Ndumbaro ameyasema hayo wakati akishiriki mkutano wa dharura wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa jumuiya ya nchi za Afrika,Caribbean na Pacific (OACPS) ambapo Tanzania inapata heshima ya kukabidhiwa Uenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa ngazi ya Balozi na Waziri katika nchi 79 za jumuiya hiyo.

Ameongeza kuwa mbali na masuala hayo pia Tanzania katika kipindi chake cha uenyekiti itatilia mkazo zaidi suala la mashirikiano ya kiuchumi ili kuziwezesha nchi zote za Jumuiya ya Afrika,Caribbean na Pacific kuingia katika uchumi wa kati ili kupunguza umasikini miongoni mwa wananchi wake jambo litakalosaidia kupunguza uhamiaji haramu na kupunguza uhalifu wa kimataifa miongoni mwa nchi hizo.

Aidha amesema kuwa hoja nyingine ni kuhusu majadiliano yanayoendelea hivi sasa kati ya Nchi za Afrika,Caribbean na Pacific na Jumuiya ya Ulaya ya kupata mkataba mpya baada ya kumalizika kwa mkataba wa Kotonu uwe ni mkataba wenye manufaa kwa pande zote mbili utakaokuwa na msukumo katika suala la maendeleo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...