Na Woinde Shizza ,Arusha

RICHARD  Paul maarufu Marcas ameomba ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kutokana na utendaji  kazi alioufanya katika jamii

Akizungumza wakati wa kuomba kura ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Paul amesema alishawahi kufanya mambo malimbali ikiwemo uanzilishi wa kukusanya mapato ya maegesho ya magari  (Parking )Mkoa wa Arusha  mbali na kazi hiyo  pia  kazi ingine aliyoifanya ni pamoja na kushauri Twiga Bank kuwa bank ya Posta mara baada ya kuona bank hiyo kuwa na matawi manne na kukusanyamadeni na baadae kuwa moja ya bank kubwa nchini

Pia amesema ni mkusanyaji wamadeni sugu mamlaka ya usimamizi wa bandari zote Tanzania pamoja na mdai ya madeni sugu ya wanafunzi wa chuo cha bandari

Amesema endapo atachaguliwa kuwa Mbunge wa Arusha hatasaidia wakina mama wanao panga bithaa bara barani eneo la frence cona wanapata maeneo ya kufanyia biashara zao mahali salama zaidi

Katika sera yake amehaidi atazungumza na watu wa national housing pamoja na viongozi wa chama na Serikali ili kupata jengo katikati ya mji kwa ajili ya kujenga City market

Amewaomba wajumbe kumpa ridhaa kwani jimbo la Arusha linaitaji mtu mwenye maono kama ya kwakwe aweze kusaidiana na John Magufuli kuendeleza Tanzania ya uchumi wa kati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...