Na Mwandishi wetu,
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga ametembelea Banda la Benki ya Maendeleo TIB wakati wa Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.

Akiwa bandani hapo alipata maelezo kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na benki hiyo.

Benki ya Maendeleo ya TIB inashiriki maonesho ya Nane Nane ili kutoa elimu kwa umma, kutangaza huduma inayozitoa pamoja na kuvutia wateja wapya kwa ajili ya uwekezaji katika miradi ya kimkakati nchini.

Pia, benki inatumia fursa hiyo kutoa ushuhuda wa miradi ya kimkakati iliyokopeshwa kwa wateja wake waliotapakaa nchini.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga akiongea na wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo TIB wanaoshiriki Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga (kulia) akisikiliza maelezo kuhusu Benki ya Maendeleo TIB kutoka kwa Meneja Masoko na Uhusiano wa Kitaasisi, Bw. Saidi Mkabakuli (kushoto). Wapili kushoto ni Afisa Mwandamizi wa Masuala ya Bima wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. James Manyama.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga (wapili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo TIB wanaoshiriki Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...