MKUU wa Mkoa wa Ruvuma
Christina Mndeme amekabidhi msaada wa taulo za kike 2,502 zilizotolewa na
Shirika la Social Action Trust Fund(SATF) kwa wanafunzi wa shule saba za msingi
wilayani Nyasa.
Mndeme amemkabidhi
taulo hizo na nguo za ndani 834 Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isebala Chilumba katika
hafla fupi iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma
mjini Songea.
Mndeme amezitaja shule
ambazo zitakabidhiwa msaada huo kuwa ni
zenye wanafunzi wa darasa la nne hadi la sita kutoka shule saba za msingi ambazo ni shule
ya msingi, Kilosa, Likwilu, Muongozo,Ukuli,Kuhamba,Liparamba na Lumeme.
“Natoa wito kwa
Halmashauri ya Nyasa,kuhakikisha inashirikiana na Shirika la SATF,kabla ya
matumizi ya vifaa wanafunzi wapewe mafunzo kupitia klabu zao za
afya.’’alisisitiza Mndeme.
Amesema kutolewa kwa vifaa hivyo ni juhudi za serikali za kuhakikisha kunakuwa na
mazingira wezeshi ya kumhakikishia mtoto wa kike anapata elimu kwa kuhudhuria
masomo na anadumu shuleni na kuhitimu masomo yake bila vikwazo.
Naye Afisa Miradi wa
SATF Makao makuu Edgar Kihwelo amesema shirika hilo linafanya kazi na Asasi za kiraia 19 katika mikoa 16 na wilaya
32 za Tanzania Bara.
Amesema tangu
kuanzishwa kwa Shirika hilo watoto
wanaishi katika mazingira magumu 193,000 wamesaidiwa na kuwawezesha kupata
elimu na kaya zipatazo 900 zimejengewa uwezo kiuchumi.
Kulingana na
Kihwelo,katika wilaya ya Nyasa kwenye mradi ulianzishwa mwaka 2019,Shirika
limeweza kusaidia watoto wa shule za msingi 103 na watoto wa shule za
sekondari sekondari 80.
Akizungumza baada ya
kupokea msaada huo ,Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba amelishukuru
Shirika la SATF kwa msaada huo ambao amesema utasaidia kumkomboa mtoto wa kike
kielimu na kufikia ndoto zao.
Kwa upande wake Afisa
Elimu Mkoa wa Ruvuma Imanuel Kisongo amelipongeza Shirika la SATF kwa kuunga
mkono jitihada za serikali za kumkomboa mtoto
wa kike katika Mkoa wa Ruvuma.
Amesema taulo za kike
zitamhakikisha mtoto wa kike anahudhuria masomo hata katika siku zake za hedhi bila kuathiri masomo
yao na kutimiza malengo yao kimaisha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...