Na Woinde Shizza, Michuzi TV ARUSHA
WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema Serikali imeamua kufuta na kuunganisha baadhi mifuko ya uwezeshaji 54 iliyopo na kubakiza michache yenye uwezo ya kuwafikia wananchi wengi vijijini
Ameeleza hayo leo wakati akifungua maonyesho ya nne ya mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi yanayoendelea Mkoani Arusha, ambapo amesema kuna mifuko mingi ambayo haijulikani nini inafanya na wapi inapatikana, hivyo Serikali haina budi kuifuta na kuunganisha baadhi ili lengo la kuwawezesha wananchi kiuchumi liweze kutumia.
Aidha amewaagiza wakuu wa mikoa kupitia mifuko hiyo kuangalia aina ya mikopo wanayotoa Ili kuweza kuwasaidia wananchi kutapata uwezeshwaji kwa gharama nafuu.
Pia ameiagiza mifuko hiyo kufanya uwezeshaji kwa kuwa wabunifu zaidi ili kuweza kupanua wigo wa kukuza uchumi wa wananchi na kwenda sambamba na malengo ya Serikali yanayolenga kukuza uchumi taifa na mtu mmojammoja.
Vilevile amesema kuwa, tathimini zilizofanywa zinaonyesha mifuko hiyo imesaidia kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kupata mikopo ambapo hadi sasa mifuko hiyo imeshatoa mikopo ya shilingi trilioni 2.22 iliyowanufaisha watu milioni 4.9.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi, Festus Limbu amesema kuwa, maonesho hayo yamekuja katika kipindi kizuri ambacho serikali imeingia Katika kipindi chake cha awamu ya pili ya uongozi ambao bado wanaendelea na dhamira yake kutekeleza kauli mbiu yao ya kuwezesha wananchi kiuchumi.
"Dhamira ya nchi katika ujenzi wa taifa imara inatekelezwa kwa nguvu zaidi na ndio maana kauli mbiu ya maonyesho hayo inayosema "Mifuko na Programu ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa Maendeleo ya Taifa." Amesema.
Amesema kuwa Serikali ilianzisha mifuko hiyo kwa ajili ya kusaidia wananchi kujenga uchumi wa nchi na kuteketeza umaskini .
Pia Katibu mtendaji wa baraza la taifa la uwezeshaji wananchi kiuchumi Beng'i Issa alisema kuwa Katika maonyesho hayo watatoa mafunzo mbalimbali ikiwemo namna ya kuandaa maandiko ya biashara, ujasiriamali, mikopo, Jinsi ya kuanzisha biashara, jinsi ya kuongeza thamani ya biashara pamoja na namna ya kutunza maandiko ya biashara.
Amesema wanategemea maonesho haya yatakuwa na manufaa makubwa katika kuelekea uchumi wa viwanda hususani katika kipindi hiki ambacho taifa limefikia mefika katika uchumi wa kati.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...